Kijue kichaa cha Mbwa
KIJUE KICHAA CHA MBWA
Na;- SHIRA S.MANGUBE
IDARA YA AFYA – KINGA
RRH – LIGULA
MALENGO YA MADA:
- Kujua kichaa cha mbwa
- Jinsi ugonjwa unavyoenea
- Muda wa dalili kujitokeza (Incubation period)
- Kufahamu dalili zake kwa mtu
- Makundi 3 ya aina ya jeraha
- Kujua jinsi ya kuhudumia mtu aliyetafunwa na mbwa mwenye kichaa
- Kujua tiba kinga inayopaswa kutolewa kwa mtu aliyeumwa na mbwa anayehisiwa kuwa na kichaa
- Kujua mbinu zinazotumika kudhibiti ugonjwa wa kichaa cha mbwa
UGOJWA WA KICHAA CHA MBWA NI NINI?
Ugonjwa hatari unaoenea toka kwa wanyama kwenda kwa binadamu (zoonotic disease)
husababishwa na virusi aina ya RNA kundi la Lyssavirus, familia ya Rhabdoviridae.
Kifo ni 100% kama mtu aliyeumwa na mbwa hatapatiwa tiba kinga
JINSI UGONJWA WA KICHAA CHA MBWA UNAVYOENEA
KWA TANZANIA MBWA NDIYE MWENEZAJI MKUU WA UGONJWA HUU KWA BINADAMU NA KWA WANYAMA WENGINE KAMA NG’OMBE NK
JINSI UGONJWA WA KICHAA CHA MBWA UNAVYOENEA
KATIKA MATUKIO MACHACHE KICHAA CHA MBWA HUWEZA KUENEA KWA:
- Njia ya hewa (Aerosolized virus)
- Kwa njia ya kupandikizwa kiungo cha mwili (Transplantation of tissue) kama figo toka kwa mtu mwenye maambukizi ya ugojwa wa kichaa cha mbwa
(TANZANIA HAIJAWAHI KUTOLEWA TAARIFA)
MUDA WA DALILI KUJITOKEZA(INCUBATION PERIOD)
Siku 10 mpaka mwaka mmoja( Wastani ni mwezi 1 hadi 2.
Hii hutegemeana na:
- Idadi ya virusi vilivyoingizwa mwilini
- Ukubwa wa eneo la mwili lililotafunwa
- Kinga binafsi ya mtu mwilini
- Aina ya kirusi kilichoingizwa mwilini
- Umbali wa jereha kutoka kwenye mfumo wa fahamu
DALILI ZA UGONJWA WA KICHA CHA MBWA
UGONJWA WA KICHAA CHA MBWA HUJITOKEZA KWA NAMNA MBILI ZIFUATAZO:
- Kupooza mwili (Paralytic rabies)
2.Kichaa moto (Furious rabies)
Hatua zote hizi mbili hutanguliwa na dalili zifuatazo:
- Homa,kuumwa kichwa,mwili kuchoka,
- kichefuchefu,kutapika, kuwashwa sehemu mtu alipoumwa na mbwa,
- kuwashwa na koo na kuwa
- kikohozi kisichotoa makohozi baada ya tukio la kutafunwa na mbwa
KICHAA BARIDI( PARALYITC RABIES)
DALILI ZAKE:
- Kuuma kwa misuli ya mwili
- Kupumua kwa tabu
- Kupooza kwa misuli ya mwili hususani miguu na mikono
- Kifo
KICHAA MOTO(FURIOUS RABIES)
DALILI ZAKE:
- Kukakamaa misuli
- Kushituka shituka
- Kuhema kwa tabu
- Kuogopa maji, upepo na mwangaza
- Kuchanganyikiwa au kurukwa akili
- Kifo
NAMNA 3 ZA MTU KUPATA MAAMBUKIZI YA KICHAA CHA MBWA (TYPE OF CONTACT EXPOSURE)
- Kuguswa au kulabwa kwenye ngozi isiyokuwa na michubuko (Touching or feeding of animals/licks on intact skin)
- Jeraha lisilotoa damu (Minor scratches or abrasions without bleeding)
- Jeraha linalotoa damu (single or multiple transdermal bites
HUDUMA YA KWANZA KWA MTU ALIYEUMWA NA MBWA
- Osha jeraha kwa maji mengi yanayotiririka na sabuni
- Osha kwa maziwa au kimiminika chochote kama maji hayapatikani
- Safisha jeraha kutumia antiseptic (k.m. dettol, spirit n.k)
- Wahi kituo cha Afya kupewa TT na tiba kinga(chanjo) ya kichaa cha mbwa
TIBA KINGA (CHANJO) YA KICHAA CHA MBWA
- Hutolewa kwa njia kuu mbili (2)
- Njia ya misuli (Intra-muscular, IM)
- Njia ya ngozi(intra-dermal, ID
Njia ya ngozi(ID) inapendekezwa itumike badala ya njia ya misuli(IM) kwa sababu:
- Humpunguzia mwathirika muda wa kuhudhuria kituo cha tiba kupata chanjo
- Gharama yake ni ndogo (chupa 1 vs 5)
- Humjengea mtu kinga ndani ya siku (7) saba
UTOAJI WA KINGA(CHANJO) YA KICHAA CHA MBWA KWA BINADAMU
Njia ya misuli(IM) haipendekezwi kwa sababu zifuatazo
- Ni njia ya gharama sana
- Mteja hupaswa kuhudhuria kituo cha tiba mara tano
- Humjengea mtu kinga baada ya siku 14
UTARATIBU WA UTOAJI WA CHANJO YA KICHAA CHA MBWA
- NJIA YA MISULI(IM) 1mlx5=5vials SIKU 0, 3, 7, 14 na 28
- NJIA YA NGOZI(ID) 0.2mlx4=0.8ml SIKU 0, 3 , 7 na 28
NB: Serum(RIG) hutolewa siku 0(40IU per Kg body-weight kwa jeraha linalotoa damu tu.
- Mtu aliyepata chanjo mwaka mmoja nyuma na akaumwa tena na mbwa, apewe SIKU 0 na 3
KINGA KWA MTU ALIYEUMWA NA MBWA ANAYEHISIWA KUWA NA KICHAA
- JERAHA LA MTU ALIYEUMWA NA MBWA ANAYEHISIWA KUWA NA KICHAA HALISHONWI, kama kushona ni lazima ifanyike baada ya muathirika kupatiwa serum(RIG)
- Muathirika apatiwe Antibiotic na sindano ya Pepopunda (T.T) kumkinga na pepopunda na magonjwa nyemelezi
CHANJO KWA MAKUNDI MAALAMU - Wataalamu wa mifugo wanaoshiriki kampeni ya uchanjaji wa mbwa
- Waokotaji wa mizoga ya mbwa waliogongwa na magari
- Wataalamu wa maabara wanaofanya uchunguzi wa wanyama wanaohisiwa kuwa na kichaa SIKU 0, 7 na siku ya 21 au 28
MBINU ZA KUDHIBITI KICHAA CHA MBWA
- Kuchanja mbwa na paka kila mwaka kwa zaidi ya asilimia 70 katika kila eneo lenye mbwa/paka
- Kudhibiti idadi ya mbwa kwenye kaya kulingana na uwezo wa kuwahudumia
- Kudhibiti mbwa wazururaji
UFUATILIAJI WA UGONJWA WA KICHAA CHA MBWA/ KUNG’ATWA NA MBWA
- Ufuatiliaji wa wagojwa waliong’atwa na mbwa anaesadikiwa kuwa na kicha hutolewa taarifa kila wiki & mwezi kwa mfumo wa IDSR (IDWE, Monthly) Ngazi ya Wizara ya Afya, Maendereo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto